Wednesday, September 18, 2013

MWANAMKE NA PETE


Palitokea mama mmoja alikuw tajiri sana.
Alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa na alikuwa akimiliki meli nyingi ambazo zilikuwa zikifuata bidhaa nje ya nchi na kuzileteta ndani.

Siku moja huyo mama aliwatuma wafanyakazi wake waende wakafate vyakula kwa ajili ya biashara kwani kulikuwa na uhaba sana wa chakula katika nchi hiyo.

Wafanyakazi walienda na waliporudi na vyakula yule mama akaviangalia na kuanza kulalamika kwamba hakuridhika na chakula kilicholetwa hivyo aliamuru wale wafanyakazi wakimwage kile chakula chote baharini ili wakafate vingine.

Wale wafanyakazi wakamshauri yule mama kwamba isingekuwa vizuri chakula hicho kumwaga kwani kama hakihitaji ni vema angewapa watu ambao wanashida ya chakula.

Lakini yule mama hakukubari ushauri ule cha zaidi alicheka kwa dharau na kuanza kejeli.
Alitoka nje ya meli akasimama juu kabisa kisha akatoa pete yake ya dhahabu aliyokuwa amevaa kidoleni mwake na kuanza kusema huku akiwa ameining’iniza ile pete kwenye vidole.

“Nimesema hicho chakula chote kimwagwe baharini kamwe siwezi kuwa maskini kwa kukimwaga hiki chakula, kama nitakuwa masikini basi hii pete itarudi tena kwenye kidole changu”, akachukua ile pete akaiachia baharini.

Wale wafanyakazi wakafanya kama walivyoamuriwa na bosi wao. Wakakimwaga kile chakula wakaenda kufata tena kingine.

Siku moja akamtuma mfanyakazi wake akamnunulie samaki mbichi kwani ana hamu ya kula samaki atakayempika yeye mwenyewe.

Hivyo alitaka akanunuliwe samaki asiyepasuliwa kwani alikuwa anataku kumtengeneza yeye mwenyewe.

Na kweli aliletewa samaki kama alivyoagiza. Akamchukua yule samaki akaanza kumpasua, alishtuka sana alipoona ile pete yake aloitupa kwenye bahari tumboni mwa yule samaki.

Toka siku ile yule mama akawa masikini wa kutupa, kwani mali zote alizokuwa nazo zilitoweka.

UJUMBE
Siku zote  tunaamini kwamba mtoaji kwa kila mtu ni Mungu. Hivyo kupata kwako wewe leo haimaanishi kwamba hao waliokosa ni kwa sababu ya uzembe wao.

Kwani kuna wanaopambana na kutafuta sana tena inawezekana wakawa wanatafuta na kuhangaika kuliko hata wewe ambaye unajiona kwamba umepata.


Hivyo si vema kutoa kejeli kwa wasiokuwa navyo na kama unaona unastahili kusaidia, saidia siyo unaweka NADHIRI.

No comments:

Post a Comment